Tuesday, June 4, 2013

Jamaa kasafiri kikazi kwenda mkoani akamuacha mpenzi wake Dar maeneo ya Mabibo.

Jamaa kasafiri kikazi kwenda mkoani akamuacha mpenzi wake Dar maeneo ya Mabibo. Baada ya kama miezi miwili hivi binti akamuandikia jamaa barua: "Bakari naona mimi na wewe mapenzi yetu yamefika mwisho. Kwa miezi miwili iliyopita nimeamua kuendelea na maisha yangu na tayari nishatoka na Beda muuza chipsi na Kalimari muuza mchele wa jumla., la msingi isiwe ugomvi, siwezi kuwa na mwanaume kama wewe usiye na mbele wala nyuma, naomba tu nitumie ile picha yangu kila mtu achape mwendo kivyake." Jamaa baada ya kuisoma roho ikamuuma sana. Akazunguka kwenye studio mbili tatu za picha akapata picha kama za wasichana 19 hivi tofauti tofauti halafu akaongeza na ya yule binti akamtumia kwa barua na ujumbe huu."Ki ukweli bado sijaelewa wewe ni Jamila yupi. Nimewahi kuwa na wapenzi wenye jina Jamila kama 20 hivi. Naomba uangalie picha yako ni ipi kati ya hizo, ichukue then zinazobaki nitumie. Goodbye!"

No comments:

Post a Comment